Leo September 20, 2016 kwenye upande wa soka nimeipata hii ya Mshambuliaji was club ya Barcelona Lionel Messi ambaye amemtaja mchezaji anayemkubali zaidi duniani, najua utakua umeshaweka jina la mchezaji unayehisi Messi kamtaja mtu wangu.
Mid fielder wa club ya Barcelona Andres Iniesta ndiye mchezaji aliyetajwa na Messi kama mchezaji anayemkubali zaidi. Iniesta na Messi wote ni zao la Academy au Team B ya club ya Barcelona, Muajentina huyo amesema japokuwa wote wana mchezo unaofanana, Bado Iniesta mwenye asili ya Hispania amekuwa na uwezo wa kipekee ambao yeye binafsi amejikuta hawezi kuufikia.
Post a Comment