Joseph Omog amedhihirisha ubora wake leo baada ya kuiongoza Klabu ya Simba kuifunga timu yake ya zamani Azam bao 1-0, katika mchezo Ligi ya Vodacom uliopigwa uwanja wa Uhuru Dar es Salaam.
Simba waliokuwa wageni kwenye mchezo huo walipambana hadi dakika ya mwisho kupata matokeo hayo ambayo yameipandisha kileleni mwa msimu kwa kufikisha pointi 13, na kuiacha Azam ikishuka hadi nafasi ya tatu na kubakia na pointi zao 10 walizokuwa nazo kabla ya mchezo huo.
Post a Comment