Watafiti nchini Marekani wamesema
wamebaini aina fulani ya samaki anayeweza kuzalisha upya uti wake wa
mgongo unapovunjika wanaweza kusaidia kubuni matibabu yatakayoweza
kuwasaidia watu waliopooza kutembea tena.
Wanasayansi wamegundua
kuwa samaki huyo ajulikanaye kama Zebra Fish anapovunjika uti wa mgongo,
huzalisha sehemu nyingine ya uti wa mgongo na kuunganisha kama daraja
sehemu zilizokatika kwa kutumia aina ya protini mwilini mwake.Wanadamu wanayo aina hiyo ya protini inayoweza kuzalisha mifupa lakini haifanyi kazi sawa na ile ya samaki huyo.
Aina hiyo ya protini kwenye binadamu inafanana kwa asilimia 90 na aina hiyo kwenye samaki hao.
Post a Comment