Unknown Unknown Author
Title: Waliowadunga watoto dawa ya heroin wakamatwa Marekani
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Familia moja katika jimbo la Washington nchini Marekania inalaumiwa kwa kuwadunga watoto wadogo sindano zenye madawa ya kulevya ya heroin...
Familia moja katika jimbo la Washington nchini Marekania inalaumiwa kwa kuwadunga watoto wadogo sindano zenye madawa ya kulevya ya heroin ili kuwafanya walale.
Polisi wanasema kuwa Ashlee Hutt na Mac Leroy McIver walipatikana wakiishi na watoto watatu wenye umiri wa miaka 6, 4 na 2 ambapo pia zilikuwepo sindano na madawa ya heroin.
Bi Hutt alifikishwa mahakamani siku ya Jumatatu ambapo anakabiliwa na kesi ya kuhatarisha maisha ya watoto
Bwana Mclver naye anakabiliwa na mashtaka kama hayo.
Kulinga na taarifa za mahakama, mtoto wa umri wa miaka sita aliwaambia wachunguzi kuwa watu hao waliwapa dawa ya kuhisi vizuri ambazo alizielezea kuwa poda nyeupe ambayo inachanganywa na maji na kudungwa kwa sindano.
Wawili kati ya watoto hao walipatikana na dawa hiyo mwilini baada ya uchunguzi pamoja na alama za kudungwa sindano

About Author

Advertisement

Post a Comment

 
Top